Ng'ari Ng'ari Lyrics - Lava Lava




Ng'ari Ng'ari Lyrics - Lava Lava


[AYOLIZER]

Nimetulizana, ndege kwa kiota sitoki
Mambo mwororo
Nimenasiana hata kwa kuku kutwa sing'oki 
Kwa minyororo

Nishasahau zamani kushikana mashati mizozo
Mapenzi gani kila kukicha vibonzo
Nimepata mwandani bila VAT bila tozo
Wambea kunani mnakipi kina mama nyonzo

Na nimeamua sitaki sitaki
Kurudia matapishi nishakula yamini divai

Aende akanishitaki mahakamani polisi
Kama kuna kitu ananidai
Ooh! Poleni wanokonoko 
Penzi linameta meta meta
Mwali fundi si kitoto
Kama kasomea veta veta
Mwiteni na kiroboto
Mje na matarumbetambeta
Sisi twachochea moto
Roho kuwakereketa

Penzi linang'ara, ng'ari ng'ari
Mtaliona hivi hivi, ng'ari ng'ari
Kwa mbali linapepea, ng'ari ng'ari
Mtaliona ivi ivi, ng'ari ng'ari
Wenyewe twajifaidia

Aniita, aniitani ayuni
Namwita, namwita nyonda sabuni
Anipa, anipa mpaka mafuli
Sio mbwembwe, ndio zake tamaduni

Najua mimi niko peke yangu 
Ndo maana natamba
Sina shaka hofu kwa raha zangu
Hata mkinichamba
Wenye roho za kwanini
Nitajijua zangu niko naye sambamba
Mi napenda yake anapenda yangu 
Kuilamba lamba

Zifikisheni salamu kwa yule kidudu mtu
Mwambie kutesa kwa zamu asipige marufuku
Yaani ni mashamu shamu leo mambo iko huku
Nimepata bekamu fundi si butubutu

Ooh! Poleni wanokonoko 
Penzi linameta meta meta
Mwali fundi si kitoto
Kama kasomea veta veta
Mwiteni na kiroboto
Mje na matarumbetambeta
Sisi twachochea moto
Roho kuwakereketa

Penzi linang'ara, ng'ari ng'ari
Mtaliona hivi hivi, ng'ari ng'ari

Kwa mbali linapepea, ng'ari ng'ari
Mtaliona ivi ivi, ng'ari ng'ari
Wenyewe twajifaidia

Mwenzenu napewa vitamu, tende halua halua
Vya pwani vya bara, tende halua halua
Anipa haninyimi wala, tende halua halua
Mwenzenu nalishwa nalala, tende halua halua
Aah...

Post a Comment

Please Select Embedded Mode To Show The Comment System.*

Previous Post Next Post

Contact Form